• Facebook
  • Twitter
  • Google Plus
  • Contact

FILM TANZANIA

FILM TANZANIA

  • Home
  • INTERVIEW
  • SIMULIZI
  • HABARI
  • BEHIND THE SCENES
  • LOCATION
  • ABOUT
    • Facebook
    • Twitter
    • Google Plus
Home » HABARI » TUKUBALI KUELEKEZANA

TUKUBALI KUELEKEZANA

Add Comment
HABARI


Script ni nini?

    Mwandishi mzoefu lazima ajue maana ya script kwa lugha yetu inaitwa mswada,wengine hupenda kuita muongozo wa filam.Script ni maandiko yenye uchambuzi kila tendo au tukio la kisauti au kitabia yenye kuonekana katika kueleza hadithi(story).
     Filam inategemea utendaji wa watu zaidi ya mmoja ili kukamilika nao ni mtunzi wa story,mwandishi wa story,mtayarishaji wa story,muongozaji wa story, wapigaji picha wahusika na wengine wengi kutokana na bajet(budget) ya filam hivyo bila karatasi au document yenye maandiko yaliyo chambuliwa na muongozo wa story inakuwa ngumu kumuelewesha muhusika kuhusu story inayotakiwa kuitendea vitendo,nchi zilizo endelea au watendaji walio makini wanaipitia script ili kufaham story nzima inavyokwenda na inahusu nini?.     


 Kwa njia hii ni rahisi kwa wahusika kuuvaa uhusika unaotakiwa atakuwa ameilewa nafasi yake kwa marefu na mapana.Muhimu kufahamu filam yako ni maalum kwa walengwa wapi usisahau hao walengwa lazima uoneshe  story  yako wakae kwa muda  kuipitia kama itakuwa kuna sehemu hajaielewa akuulize sio awahadithie alafu siku ya kuanza kazi ndio awapatie script, Pia script yako unatakiwa uichambue vitu ambavyo vinaweza kuonekana na walengwa au watazamaji  [audience] sio wasikie vikihadithiwa.
   
   Uandisshi wa muongozo wa filamu muswada [script] unatakiwa unao vitu vya kuonekana au kuoneshwa  kuliko kuhadithiwa au kusikika  [mfano] Muhusika anamuhadithia tukio alilolipata au aliloliona likiwa katika hiyo filamu hilo tukio halijaoneshwa,kinyume chake itapelekea story yako kutokuwa na mvuto kutokana na simulizi nyingi kuliko vitendo vyenyewe vinavyosimuliwa ndani ya hiyo filamu.                                Siku zote filamu ni sanaa inayoonyesha story ya mtu au kitu ili filamu ipendwe lazima iwe na story nzuri wahusika waitendee  haki kama tukio linalofanyika kweli hata mtazamaji akimaliza kuiangalia awe amehusika kwa kuifikiria na ajiulize kama angekuwa yeye pia asijilaumu amepoteza pesa kuinunua filamu yako.                   Story nyingi zipo ndani ya kanuni na kanuni yake ndani ya story lazima awe muhusika na hitaji.Muhimu kuweka kisa kizuri kionekane kina uhalisia zaidi ili iwe rahisi kueleweka kwa walengwa wako,kisa chako kimpelekee mhusika mkuu kukaa katika nafasi yake na kuwashawishi watazamaji kumpenda na kumwonea huruma au kumpongeza kwa utendaji wake mzuri katika hiyo filamu hapo ndipo kwenye moyo wa filamu.
     
   Kisa ni kitu kinampelekea muhusika wako mkuu asifikie lengo lake kwa mikiasa na misukosuko anayoyapata muhusika wako mkuu usimpeleke haraka katika lengo lake lazima upitie majaribuni nao watazamaji wa filamu wanyanyuke kwa hisia hapo ndipo mtazamaji ataacha shughuli zake na kuwa mkini katika hiyo filamu baadhi watazamaji wanaokuwa wapole hata kuongeleshwa hataki, hakikisha unakuwa na  visa vidogo vidogo ambavyo vinazaa matukio yatakayomfanya muhusika wako mkuu anazidi kudidimia, kila atakaposhika kwa moto huruma na upendo kwa muhusika mkuu utatoka kwa watazamaji.
           Filamu itakuwa na mvuto zaidi kama utapangilia vizuri visa na mtiririko mzuri wa mtukio halisi yenye kuvutia na kutomtoa muhusika mkuu katika lengo lake kuu na sio mbaya ukawaweka watu watakao msaidia muhusika mkuu katika lengo lake hao wasaidizi wake watamwongezea nguvu  katika hitaji lake ila usimkimbizishe au kumtoa kwenye tatizo ulilomwekea.Kisa hiki ni kitendo  au tukio lolote ambalo linaloongezeka na kuleta vizuizi upingamizi na ugumu katika safari ya kufika katika lengo ambalo ndilo hitaji la muhusika kwa kuzingatia vitu hivyo tutazame muundo maarufu sana katika uandisi wa miongozo ya filamu, muundo huu pia hutumika katika uandisi wa vitabu vya tamthilia riwaya na michezo au maijizo ya luninga kufahamika three act structure [vitendo vitabu vya muundo].  Mfano
                                                           

0 Response to "TUKUBALI KUELEKEZANA"

← Newer Post Older Post → Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

FOLLOW US

POPULAR POSTS

  • KILA MWANDISHI WA MISWADA {SCRIPT}
    Kila mwandishi wa miswada {script} hutumia njia aipendayo kuitumia katika kuandika miswada {script}si kwa nchi yetu ya Tanzania pekee h...
  • IFAHAM HISTORIA YA KANUMBA YOTE KWA UJUMLA
    Hayati Steven Kanumba amezaliwa Januari 8 ,1984 Shinyanga,Tanzania Amefarki Aprili 7, 2012 (umri 28)Dar es Salaam,Tanzania Kaz...
  • SAMAKI MTU(MERMAID) 01
                                                                                                             SAMAKI MTU(MERMAID)   ...
  • MZEE MSISIRI ATUMBUA JIPU
    •••• ♦ •••• ♦ •••• ♦ •••• ♠ ••• ♦ 1. Jina langu kamili ni FADHILI RAJABU MSISILI 2. Kabira langu ni Chotara wa kizigua kwa baba na ...
  • SAMAKI MTU(MERMAID) 04
                                                                                                                          SAMAKI MTU(MERMAID...
  • ULINGO WA MOTO FILAM YA MAPIGANO YENYE UARISIA
    Daaah!!! Nikali tena ni noma sana,Usisa hau wala usikose kupata nakala yako.Tarehe 23/4/2018 filamu hii itakua tayari imo sokoni.....UL...
  • SAMAKI MTU(MERMAID) 02
                                                           SAMAKI MTU(MERMAID)                                                        ...
  • MFAHAM JUMA KILOWEKO SAJUKI
    Sajuki alizaliwa mwaka 1984, mkoani Songea na kupata elimu yake ya msing na sekondari hukohuko mkoani Songea.Ambapo mwaka 2005 aliweza ku...
  • JINSI YA KUTENGENEZA FILAM NA KUUZA
     KATIKA miongo kadhaa iliyopita filam nyingi zenye mafanikio zimetokezwa huko Hollywood. Hilo limekuwa na uvutano mkubwa ulimwenguni pote ...
  • SAMAKI MTU(MERMAID) 11
                                                                   SAMAKI MTU(MERMAID)                                                 ...
Back to top!
Copyright (c) 2014 FILM TANZANIA. All Rights Reserved Created by Flash TZ Blog. Designed by Flash TZ Blog. Powered by Blogger.